CHATANDA AFICHUA SIRI YA USHINDI WA DKT. SAMIA UCHAGUZI WA OCTOBA MWAKA HUU.


Na : Stella Ngenje-Songea.

Wananchi  Wilayani Rufiji Mkoani Pwani wametakiwa Kujitokeza kwenye Vituo vya Kupigia Kura ili kujiandikisha nakuboresha Taarifa zao kwenye Daftari lakudumu la Mpigakura litakapowafikia kwa awamu ya pili,akiwasihi pia kujitokeza kupigakura Baadae Mwaka huu.


Ameyasema hayo Mwenyekiti wa Jumuiya ya Umoja wa Wanawake  wa Chama cha Mapinduzi Tanzania UWT  Ndg.Mary Chatanda (MCC) akiwa Ziarani Mkoani Pwani ,ametumia nafasi hiyo kuhamasisha  Wanawake Kujiandikisha, "Hamasisheni Wanaume wajiandikishe, na Vijana Wajiandikishe ili ikifika siku yakupigakura Octoba wampigie Dkt. Samia, Wanaosema Uchaguzi Hautakuwepo wanapoteza muda tunawaomba Wala wasijisumbue Dkt.Samia Mitano Tena".


Akiwa  Rufiji Chatanda ameeleza  Mafanikio Makubwa yaliyoletwa na Serikali ya awamu ya Sita ya  Mhe.Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan, ameimarisha Sekta Mbalimbali ili kuondosha adha kwa Wananchi wa Rufiji, Mathalani Kwenye  Sekta ya  Elimu,Afya,Maji Miundombinu ya Barabara  Sambamba na  uwezeshaji Wananchi kiuchumi.


Ziara  hii Mkoani  Pwani pamoja na Mambo Mengine, Chatanda amesema inalenga  Kukagua  Utekelezaji wa Ilani ya CCM, akimtaja Dkt. Samia  Kuwa ni  "Mwanamke na Nusu" na kwamba anastahili Pongezi kwa Maendeleo Makubwa aliyoyaleta kwa Mikoa Mbalimbali hapa Nchini, Ikiwemo na Mkoa wa Pwani.








🚨Full VIDEO inapatikana kwenye YouTube Channel yetu ya WASHINDI MEDIA.

Previous Post Next Post