Waziri Kairuki
ameyasema hay oleo Juni 5,2023 alipokuwa akizungumza na Waandishi wa habari
katika Ofisi za TAMISEMI Jijini Dodoma.
Waziri Kairuki amesema waajiriwa
wapya wanatakiwa kuripoti katika Ofisi za Wakurugenzi wa Halmashauri huku
wakiwa na viambatanishi kikiwemo kitambulisho cha Taifa au namba ya utambulisho
wa NIDA,Cheti halisi cha kuzaliwa,Vyeti halisi vya kidato cha Nne,Sita,Chuo
Kikuu,NACTE,Leseni haina Vyeti halisi vya Mabaraza ya Kitaaluma ili kuhakikiwa
na mwajiri kabla ya kupewa barua ya uajiri.
“Mtakumbuka mwezi April
2023 Mhe.Dk.Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania alitoa
kibari cha ajira kwa watumishi 21,200 kati yao 13,130 walikuwa wa kada ya
ualimu na 8,070 wa kada ya Afya.
“Baada ya kupata kibari
cha ajira Ofisi ya Rais TAMISEMI ilitoa taangazo kwa wahitimu mbalimbali kwa Walimu
na kada za Afya kuwasilisha maombi ya kazi kupitia mfumo wa kielektroniki
kupokea na kuchakata maombi ya ajira kuanzia tarehe 12/04/2023 hadi 25/04/2023.
Pia Waziri Kairuki amebainisha
kuwa Ofisi ya Rais TAMISEMI iliunda timu maalumu ya uchambuzi ambayo ilifanya
kazi ya kuchambua na kuhakiki maombi mbalimbali ya ajira ambapo uhakiki huo
ulifanyika katika hatua mbalimbali kutokana na idadi ya waombaji kuwa kubwa.
Amesema timu hiyo
iliainishiwa vigezo vya kuzingatia katika mchakato wa uchaguzi wa waombaji
ajira ili kuhakikisha kunakuwepo na haki na uwazi katika zoezi hilo ikiwa ni
pamoja na mwaka wa kuhitimu kikiwa ni kigezo kilicho zingatiwa,kigezo cha umli
wa kuzaliwa, pamoja na uchambuzi wa watu wenye ulemavu.
Amesema mchakato wa
uhakiki na uchambuzi wa kada za afya na ualimu ulifanywa kwa awamu mbili ambapo
uhakiki wa awali ulifanywa kwa mufumo na kati ya maombi 171,919
yaliyopokelewa,waombaji 49,089 waliondolewa kwenye mchakato hali iliyofanya
kubaki na waombaji 122,827.
Hata hivyo ameeleza
kuwa waombaji walioondolewa awali ni 1456 waliomba nafasi za ualimu wakiwa
wamehitimu kabla ya mwaka 2015 huku waombaji 47,633 waliomba masomo ambayo
hayakutangazwa katika matakwa ya tangazo la ajira.
Pamoja na hayo Waziri
Kairuki amesema baada ya zoezi la uhakiki wa waombaji wa kimfumo na mapitio ya
nyaraka jumla ya waombaji 86,448 walikidhi vigezo na hivyo kuingizwa katika
mchakato wa kupangiwa vituo vya kazi ambapo kati ya waombaji 86,448 waliokidhi
vigezo waombaji wa kada za afya ni 21,273 ambapo kati yao wanawake ni 10,618 na
wanaume ni 10,655.
Amesema waombaji
wa kada za elimu ni 65,175 walikidhi vigezo ambao kati yao wanaume ni 38,584 na
wanawake ni 26,591.
“Waombaji 86,448
waliokidhi vigezo na sifa walitakiwa kujaza nafasi za kazi 21,200 walimu 13,130
na afya ni 8,070 kwa mjibu wa kibali kilichotolewa,”Waziri Kairuki
Aidha amesema kwa waajiriwa
wapya watakao chukua posho ya kujikimu na baadae kukiuka kuripoti katika maeneo
yao ya kazi waliyopangiwa watachukuliwa hatua stahiki kwa mjibu wa sheria ikiwa
ni pamoja na kushitakiwa kwa kosa la kujipatia fedha au mali kwa njia ya
udanganyifu.