DK.MPANGO ATOA MAAGIZO KWA NEMC NA HALMASHAURI ZOTE NCHINI


Makamu wa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dk.Philp Mpango ameliagiza Baraza la Taifa la Uhifadhi na usimamizi wa Mazingira (NEMC) pamoja na mamlaka za Serikali za mitaa nchini kote kusimamia na kuongeza nguvu katika utekelezaji wa katazo la matumizi ya mifuko ya plastiki.

Dk.Mpango ameyasema hayo mapema hii leo Juni 05,2023 alipokuwa akizungumza na wananchi katika viunga vya Soko la Machinga Complex Jijini Dodoma katika kilele cha maadhimisho ya wiki ya mazingira Duniani.

Amesema Mamlaka zinatakiwa kuchukua hatua za kisheria kwa wale wanaoenda kinyume na maagizo ya ya Serikali katika kusimamia vyema suala la matumizi ya mifuko ambayo haija thibitishwa huku akiwataka watendaji wanao husika kusimamia kwa ukaribu uzalishaji wa mifuko mbadala.

Dk.Mpango amesema mamlaka inatikiwa kuhakikisha mifuko inayozalishwa inaonesha taarifa ya mzalishaji yaani anuani,eneo inapo zalishwa pamoja na kudhi viwango vilivyowekwa na mamlaka husika.

“Tuache mazoea ya kutupa taka ovyo sio usitaarabu kufanya kila eneo liwe jalala la kutupa taka ni lazima sasa tujenge mazoea ya kuyaweka mazingira safi na kwa wale walioko mazingira ya mjini ni vema kila kaya iwe na sehemu mahususi ya kuhifadhia taka au kuchoma taka,”Dk,Mpango amesema 

Pia Dk.Mpango amezitaka Kampuni na watu binafsi wanaozalisha bidhaa za plastiki kuahikisha wanakusanya taka zinazozalishwa na kuondolewa huku akisisitiza suala la utupaji taka kiholela.

Adha Makamu wa Rais Dk.Mpango amewataka pia Wamiliki wa Mabasi na magari binafsi kuweka utaratibu na kuwa na vifaa vya kuhifadhia taka katika magari yao ili kuzuia abiria kutokutupa taka ovyo wawapo barabarani na katika vyanzo vya maji.

Katika hatua nyingine Dk.Mpango amesema kwa mjibu wa kifungu cha 89  sheria za Serikali za Mitaa,mamlaka za miji sura ya 288 Halmashauri zimepewa mamlaka ya kutunga sheria ndogo za utunzaji wa mazingira na udhibiti wa taka.

Hata hivyo amesema licha ya kuwepo kwa sheria hizo bado kunatatizo la usimamizi na utekelezaji wa sheria hizo na kuziagiza Halmashauri zote nchini kuandaa utaratibu katika kusimamia sheria ndogo zilizotungwa na Halmashauri na kuhakikisha hatua za kisheria zinachukuriwa dhidi ya watu watakao kiuka sheria hizo.

   

 

 

Previous Post Next Post