Rais wa Jamuhuri ya
Muungano wa Tanzania Dk.Samia Suluhu Hassan amewataka watanzania na mashabiki
wa michezo kuweka mbele uzalendo katika michezo kwa maslahi ya Taifa.
Dk.Samia ameyasema hay
oleo Juni 5,2023 wakati wa hafra ya chakula cha usiku ya kuipongeza Timu ya
Yanga kwa hatua waliyoifikia ya kucheza Fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika
(CAF)iliyofanyika katika ukumbi wa Jakaya Kikwete,Ikulu Jijini Dar es salaam.
Hata hivyo amesema
hatua ya Timu ya Yanga kufika kwenye mashindano ya CAF imeleta heshima na
kurejesha nchi katika ramani ya kisoka na michezo kwa ujumla.
Pia amewapongza wapenzi
na mashabiki wa timu ya Yanga kwa hamasa waliyokuwa wakiitoa kwa wachezaji wa
Yanga wakati wa mashindano hayo.
Aidha Dk.Samia ametoa
wito kwa Serikali za mitaa kote nchini kuweka mkazo katika michezo na kuwa na
viwanja katika maeneo yao.
Tags
MICHEZO