WANAWAKE WAJASILIAMALI WAPEWA SEMINA,WATAKIWA KUCHANGAMKIA FURSA

Na Fedrick Mbaruku

NAIBU Waziri wa kilimo na (Mb) wa Dodoma Mjini Mhe.Antony Mavunde amewataka akinamama wajasiliamali kuchangamkia fursa mbalimbali za kiuchumi ili kuleta mabadiliko chanya katika taifa na jamii kwa ujumla.

Mhe.Mavunde ameyasema hayo hii leo Juni 9,mwaka huu wakati alipokuwa mgeni rasmi kwenye semina ya akinamama wajasiliamali katika hafla ya uzinduzi wa program ya “She can do it” iliyohusisha  ugawaji wa hati za umiliki wa ardhi iliyofanyika katika ukumbi mdogo uliopo PSSSF Jijini Dodoma.

Amesema kwa mjibu wa sheria ya manunuzi ya umma iliyofanyiwa marekebisho anaelea bayana kuwa taasisi zote nunuzi zinatakiwa kutenga asilimia 30 ya manunuzi yake ya ndani kwa lengo la kuyainua makundi maalumu wakiwemo akinamama,vijana na watu wenye ulemavu.

Amesema katika ujenzi wa mji wa serikali Jijini humo zimeingia shilingi Bilioni 300 ambazo zipo kwenye mzunguko zitakazo tumika katika ujenzi wa mji wa serikali zinazotoa fursa mbalimbali kwa akinamama wajasiliamali,vijana na watu wenye ulemavu.

“Fursa hizi zipo lakini je wakowapi hao watu wakufanya hivo nataka niwaombe mama zangu ya kwamba tuzichangamkie hizi fursa na inawezekana kabisa tunayo miradi mingi hapa Dodoma na kama mko teyari mimi Ofisi ya Mbunge iko wazi na niko teyari kumshika mtu mkono nikampeleka sehemu husika akaendelea na mpango huu uliopo.

Mhe.Mavunde amesema Dodoma ndio sehemu pekee kusini mwa jangwa la sahala huku akibainisha kuwa kunaujenzi wa barabara ya mzunguko yenye kilometa 112.3 ambayo itakuwa na takribani njia nne itakayo chochea maendeleo katika Jiji la Dodoma na maeneo mengine hapa nchini.

Hata hivyo Mhe.Mavunde amepanga kuwalipia akinamama wajasiliamali ghalama za kujiunga katika suala zima la ujasiliamali ili kushiriki katika maonesho ya sabasaba yanayotarajia kufanyika July 7,mwaka huu huku akisema akinamama wanao wigo mpana wa kubadilika kiuchumi.

Amesema kutokana na ujenzi wa uwanja wa Ndege wa kimataifa uliopo Jijini humo unatarajia kuleta fursa itakayowawezesha wajasiliamalia kusafiri biashara zao kwa urahisi hali ambayo itawafanya kuendesha shughuli zao kwa ufanisi.

Mhe.Mavunde amesema Reli itakapo kamilika kutakuwa na uwezekano wa kusafirisha biashara zao kwa haraka sana na kwa muda mchache huku akiahidi kuwaunga mkono akina mama wajasiliamali Jijini humo.

“Kwa haya anayoyafanya Mama yetu Dk.Samia Suluhu Hassan labda mshindwe nyie na mimi niko teyari kumsaidia mtu yeyote atakae hitaji msaada kwa ajiri ya kukuza na kuleta maendeleo.

“Nimetoa ofa kwa mfanyabiashara yeyote kupitia sido nitatoa shilingi Milioni 20 kila mwaka ili nitakapoondoka kiwepo kitu kitakachoonekana na kikumbukwe kuwa na Fulani aliacha hiki,”Mhe Mavunde

“Hakuna mtu anaepewa rifti akiwa amekaa nyumbani kwake jamani ukitaka rifti sogea barabarani ebu sasa hivi tuanze kumnyenyua mtu mmoja mmoja tuone ili kesho na keshokutwa tuone mafanikio yao.

Nae Festa Mbaga kutoka kampuni ya Akili mia ametoa wito kwa akina Mkoani humo kujua mahali,hatua mbalimbali zinazotakiwa kufuatwa ili kupata mikopo na namna ya kurejesha katika taasisi mbalimbali za kifedha hususani katika Benk.

Mbaga amewasihi akinamama hao kuwa waaminifu katika sehemu wanazokopa fedha hizo huku akionya tabia ya watu kukopa kasha kasha kutokomea kusiko julikana ba badala yake kujenga uaminifu ili kufikia hatua kubwa zaidi katika kutimiza adhima aliyojiwekea mhusika.

Amoni Mabusi ambae ni Meneja wa Benki ya NMB tawi la Dodoma na Kanda ya kati amesema wajasiliamali wengi si watanzania pekee ambapo wanakabiliwa na changamoto ya ukosefu wa mitaji huku akiwasihi wajasiliamali kuwa na lughu nzuri ya kibiashara hali ambayo inaweza kukufanya biashara isikuwe.

Amesema katika suala la ujasiliamali biashara inahitaji usimamizi wa hali ya juu na kusema mara nyingi wasimamizi na wataalamu wa biashara wanashauri kuwa unatakiwa kuwa msimamizi wa karibu katika biashara.

Pia amewashauri kuwa makini katika majanga ya kibishara yanayoweza kujitokeza pindi mfanyabiashara anapoendesha shughuli zake ikiwa ni pamoja na majanga ya moto,wizi,kunyeshewa na mvua kasha kutafuta suluhisho kwa haraka juu ya majanga hayo.

“kama unaduka ni la milioni 20 halafu likaungua maana yake milioni 20 zimeungua sasa maana yake ni kwamba unatafuta milioni 20 tena usimamishe biashara kama ile kwahiyo kuna haja kubwa ya kuitengenezea lisk ili ikitokea usije ukatafuta hela nyingineza kufidia pale unaweza ukawa na bima na mengine.

 

Previous Post Next Post