SERIKALI KUTEKELEZA MPANGO WA MAENDELEO ENDELEVU NCHINI


SERIKALI Kupitia Wizara ya Fedha na Mipango imepanga kutekeleza Ajenda ya maendeleo endelevu ambayo pamoja na Mambo mengine imeainisha malengo 17 ya Maendeleo ambayo kwa kifupi yanajulikana Kama SDGs malengo hayo yanaonesha shabaha ambazo Dunia inategemea kufikia ifikapo mwaka 2030  

Kauli hiyo imetolewa leo Juni 8 Jijini Dodoma na naibu katibu mkuu wizara ya Fedha na Mipango  Jennifer Omolo  kwenye hafla ya uzinduazi wa ajenda ya maendeleo endelevu yenye lengo na mkakati wa kukuza Uchumi na Kupunguza Umasikini kwa upande wa Tanzania  bara ambao ni maarufu   Kama FYDP na ZADEP kwa upande wa Zanzibar.
Amesema kufuatia ujumuishaji huu mipango pamoja na bajeti zote za kisekta zimeendelea kuasili na kutumika Kama nyenzo kuu ya serikali ya utekelezaji wa afua za SDGs ilikuongeza Kasi utekelezaji wa SDG na kufuatilia malengo yote 17
"Serikali kupitia ofisi ya takwimu iliainisha maendeleo ya kijamii tukizungumza swala la maji tunataka watu wajue serikali imepambana kwa kiasi gani kutoka kutoka miaka ya nyuma na Sasa tukizungumza Afya tunamanisha taarifa za mapitio zinapaswa kusimamiwa na serikali pamoja na tasisi binafsi,"

Tanzania inapaswa kuwasilisha katika jukwaa kuu la kisiasa nchini marekani V.N.R  mchakato wa kufanya utafiti wa SDGs linajumuisha sekta zote pamoja na taasisi "ameeleza Jennifer 

Naye Naibu Katibu Mkuu wizara ya Elimu  Sayansi na Teknolojia Bw Frank Rozamula amesama kutokana na utekelezaji wa malengo ya maendeleo endelevu wizara ya Elimu inagusa kila mtu na inazingatia ubora wa Elimu na inwafikia na kuwafikaa  watanzania

"Wizara ya elimu tumefanya Mambo mengi Kwanza tumejenga miundombinu Kama  madarasa kwa shule za msingi na shule za sekondari ilikuhakikisha watoto hawapati shida sehemu ya kujifunzia pamoja na vitabu lakini tumetoa mafunzo kwa walimu walio shuleni na walio mafunzoni tumetoa vishikwambi kwa walimu,

"kwa upande wa elimu ya juu tumejenga kampasi 17 katika mikoa minne ilikufikia maeneo ambayo hayana vyuo vya Kati na kila mkoa tumepanga kujenga shule ya watoto wa kike na kila shule itakuwa wa wanafunzi 1000"ameeleza Rozamula

Previous Post Next Post