WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA AMEIPONGEZA OFISI YA WAKILI MKUU WA SERIKALI KWA KUOKOA ZAIDI YA SH.TRILIONI SABA

WAZIRI Mkuu wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Kassim Majaliwa Majaliwa ameipongeza Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali kwa kuendesha mashauri ya madai na usuruhishi ndani na nje ya nchi kwa niaba ya Serikali na taasisi zake kwa umahiri mkubwa weledi na kuisaidia Serikali kuokoa zaidi ya trilioni saba kutokana na kutatua migogoro kwa ajiri ya usuruhishi.

Wazir Mkuu ambaye alikuwa mgeni rasmi katika maadhimisho ya miaka mitano tangu kuanzishwa kwa Ofisi 2018 na kufungua mafunzo kwa Mawakili wa Serikali yaliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Jakaya Kikwete Jijini Dodoma.

Waziri Mkuu amezielekeza Wizara,Idara na Taasisi zote kufanya kazi kwa karibu na Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali katika uendelezaji wa mashauri hayo huku akizitaka Taasisi za umma zenye Mawakili wa Serikali kuzingatia utatuzi wa kero za Wananchi ili kupunguza mlundikano wa mashauri ambayo hayana ulazima wa kufikishwa Mahakamani.

Awali akizungumza kabla ya Waziri Mkuu,Waziri wa Katiba na Sheria Mhe.Dkt.Damasi Ndumbaro amemueleza Waziri Mkuu Mhe.Kassim Majaliwa aliyekuwa mgeni rasmi kuwa Wizara itaendelea na utekelezaji wa kampeni ya kitaifa ya msaada wa kisheria hapa nchini ijulikanayo kama “Mama Samia Legal Aid Campaign” ili kutoa elimu kwa Wananchi kuhusu masuala ya kisheria kwa lengo la kupunguza mlundikano mashauri na migogoro Mahakamani.

Kwa upande wake Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mhe Jaji .Dkt.Elieser Feleshi amesema uamzi wa kuanzisha Ofisi hiyo ni kuimalisha sekta ya sheria nchini hususani katika kuongeza ufanisi zaidin katika uendeshaji wa mashauri ya madai na usuluhishi nchini.

Amesema hatua hiyo imeisaidia Serikali kuokoa fedha nyingi ambazo zinaenda kutekeleza miradi mbalimbali ya kimaendeleo nchini kwa manufaa ya Taifa.

Katika hatua nyingine ameeleza kuwa kuhusu  ushirikiano uliopo kati ya Ofisi yake na Ofisi ya Wakili Mkuu  wa Serikali,Mhe.Jaji Yohane Massara,Jaji kiongozi Mahakama ya Afrika Mashariki amasema Ofisi yake itaendelea kutoa ushirikiano ili kufikia hatua kubwa zaidi.

Pia ametoa rai kwa Wakili Mkuu wa Serikali kuendelea kutoa mafunzo kwa Mawakili wengine wa Serikali sio tu kwa mafunzo yanayohusu uendeshaji wa kesi za madai na usuluhishi hapa nchini laikini pia katika mahakama za kikanda na za kimataifa ili kuwa na muendelezo wa mawakili wengine katika kuitetea Serikali mara tu baada ya walipo kusitaafu.

Aidha Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe.Rosemary Senyemule ameipongeza Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali kwa utendaji kazi mzuri na kumpongeza Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dk.Samia Suluhu Hassan kwa dhamira aliyonayo kwa kila sekta ikiwa ni pamoja na sekta ya sheria na taasisi zake katika kuahakikisha kuwa kila mwananchi anakuwa na haki kupitia vyombo vya kisheria hapa nchini.  

Previous Post Next Post