NDEGE YA MIZIGO YAPOKELEWA,PROF.MBARAWA AAHIDI MABADILIKO CHANYA

Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dk.Samia Suluhu Hassan akiambatana na Viongozi wengine Wakuu wa Seikali ya Jamuhuri akiwemo Rais wa Zanziba na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussei Ali Mwinyi,Makamu wa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzanai Dk.Philp Mpango,Waziri Mkuu Kassim Majaliwa Majaliwa pamoja na Mke wa Makamu wa Rais Mama Mbonie Mpango na Mke wa Rais wa Zanzibar wameshiriki katika hafla ya mapokezi ya Ndege ya mizigo iliyorushwa na Rubani mmoja mtanzania Neema Swai kutoka nchini Marekani.




 WAZIRI wa Ujenzi na Uchukuzi Prof.Makame Mbarawa Serikali kupitia Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi itaendelea kusimamia uwekezaji mkubwa uanofanywa na Serikali ili miradi itumike katika kuboresha maisha ya Wanzania.

Prof.Makame Mbarawa ameyasema hayo hii leo Mei 3,2023 katika hafla ya mapokezi ya Ndege ya mizigo aina ya Boelng 767-300F iliyongozwa na Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dk.Samia Suluhu Hassan katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (Terminal One) Jijini Dar es salaam.

Amesema Serikali kupitia Wizara hiyo imekuwa ikitoa kipaumbele katika kughalamia utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo nchini.

“Katika hili Serikali kupitia Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi itaweka katika Viwanja vya Ndege vyote muhimu hapa nchini kikiwemo kiwanja cha Ndege cha Dodoma,Kigoma,Mpanda,Tabora ,Songea,Msoma na vingine vilivyopo katia maeneo mengine.

Prof.Mbarawa alisema ujio wa Ndege hiyo utaenda kuwa chachu ya biashara kati ya Tanzania na mataifa mengine na kusema adhima hiyo itaendana na utekelezaji wa farsafa ya Dipromasia ya uchumi ambayo imekuwa ikisisitizwa na Mhe.Rais Dk.Samia Suluhu Hassan sambamba na mahusiano kati ya Tanzania na mataifa mengine Duniani.

Alisema Wizara itaendelea kutekeleza majukumu yake makuu na kuandaa sera zitakazo saidia matumizi ya rasilimali kupitia uwekezaji unaofanywa na serikali ili kuleta matokeo chanya katika ukuaji wa shughuli za kiuchumi nchini.

Sanjali na majukumu hayo Prof.Mbarawa alisema Wizara itaendelea kujenga mazingira wezeshi katika sekta za kiuchumi na kijamii na sekta binafi katika kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi na weredi wa hali ya juu.

“Sekta ya usafilishaji inaleta uhai katika shughuli za kiuchumi kama ilivyo damu katika mwili wa Binadamu.

“Kwa kutambua hilo tutaendelea kushirikiana na sekta binafsi zinazo zalisha mizigo ili kuhakikisha mizigo hiyo inafika kwa haraka katika masoko mbalimbali Duniani,”alisema

Hata hivyo Prof.alisema kupitia bajeti iliyowasilishwa kwa mwaka wa fedha 2023/2024 ATCL imeongezewa Ndege,kuboresha kalakana ya matengenezo ya Ndege na uendeshaji wa shughuli za huduma za Ndege na mizigo huku akisema uwezeshaji huo unalenga kupunguza gharama za uendeshaji za ATCL ili kuiwezesha kampuni hiyo kuhimiri ushindani katika soko la anga.

Alisema Wizara hiyo kupitia Serikali itaendelea kusimamia uboreshaji wa Viwanja na miundombinu mbalimbali ili kuwezesha mashirika ya Ndege ndani na nje ya nchi kuendelea kutoa huduma kwa ufanisi zaidi.

Aidha Prof.Mbarawa aliishukuru na kuipongeza Serikali kwa kuendelea kuiboresha ATCL katika nyanja mbalimbali za kusafirisha abiria na mizigo.

Akitoa taarifa ya Ndege hiyo Mtendaji Mkuu wa ATCL Lardslaus Matindi alisema mpango wa Ndege za mizigo umelenga kurahisisha usafirishaji wa bidhaa kutoka na kuingia nchini.

Alisema ujio wa Ndege hiyo utasaidia kuongeza mnyororo wa thamani wa bidhaa za kitanzania hususani katika uwepo wa usafiri wa uhakika wa bidhaa na vifaa vinavyotumika katika uzalishaji na kuzifanya kuwa shindani zaidi katika soko la kimataifa.

Alisema katika kutekeleza mpango  mkakati wa pili wa Kampuni ya Ndege Tanzania ndani ya kipindi cha miaka mitano kwa mwaka wa fedha 2022/2023 hadi 2026/2027 inatakiwa kuwa na Ndege takribani 20 zikiwemo ndege za masafa mafupi 8,masafa ya kati 8,masafa marefu 3 na Ndege moja kubwa ya mizigo.

Aidha Matindi Alisema mapokezi ya Ndege hiyo kumeifanya ATCL kuwa na Ndege 13 zilizopo nchini na Ndege tatu zikiendelea kuundwa wakati Ndege mbili kati ya hizo tatu  aina ya Boelng 737-9MAX zinztzrzjiwa kuwasili nchini kati ya mwezi wa nane na mwezi wa 12 mwaka huu huku Ndege ya tatu Boelng 787-8 ikitarajiwa kuwasili 2024.

 

Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dk.Samia Suluhu Hassan akiwa na Rubani iliye ifikisha Ndege mpya aina ya Boelng 767-300F kutoka Nchini Marekani Neema Swai.

Previous Post Next Post