DOMECO Vs HOMEBOYS MBABE AKOSEKANA


 Itakumbukwa Mei 5 mwaka huu DOMECO ilichuana na timu ya Homeboys katika uwanja wa Shule ya Msingi Kazikazi na leo Timu hizo zimekutana kwa ajiri ya mchezo wa kirafiki Jijini Dodoma..

Mchezo huu umechezwa leo Mei 2 2023,katika uwanja wa Shule ya Sekondari City uliopo Jijini Dodoma ambapo katika mchezo huo timu zote zikiwa na ushindi wa bao 1-1 Homeboys wakitangulia kupata gori la kwanza katika kipindi cha kwanza dakika ya 42 lililofungwa na mchezaji Yohana Jackson huku DOMECO wakifuatia kupata gori katika kipindi cha pili lililofungwa na Barakia Bosco Iputa.

Michuano hiyo inakuja mala baada ya DOMECO kuifuata timu ya Homeboys ya Itigi Mkoani humo mchezo uliochezwa Mei 5 mwaka huu ambpo DOMECO walitoka na ushindi wa bao 2-1,na leo Itigi imefunga safari kuifuata DOMECO Jijini Dodoma na na kutoka sale ya bao moja kwa moja na hadi kutamatika kwa mchezo huo timu zote zikiwa na majeruhi mmoja.

Waliopata majeraha ni Ramadhan Mtapila mchezaji wa Timu ya DOMECO katika dakika ya 55 na Paschal Christopha kutoka katika Timu ya Homeboys dakika ya 54,kwa mjibu wa taarifa za awali Viongozi wa Timu hizo wameiambia Mapinduzi Digital kuwa majeruhi wanaendelea vizuri tangu walipo patiwa huduma za awali.

Akisimulia mtanange huo Nahodha wa timu ya DOMECO Barakia Iputa amesema kilichosaidia wao kurudisha gori ni matumizi ya mbinu walizokuwa nazo huku akisema mpira ni mbinu.

“Kutangulia kufungwa sio sababu kitu unachotakiwa ufanye ni mentainence walishazowea kutufunga gori la kwanza tunachomoa tunawapiga kwahiyo mchezo kama huu wa leo wametufunga gori la kwanza lakini tumewasoma akili yao maneno mengi vitendo hakuna.

Previous Post Next Post