DOMECO WAZINDUA TAWI LA UVCCM DODOMA,WATAKIWA KUWA WAZALENDO


 MWENYEKITI Wa Seneti ya Vyuo na Vyuo Vikuu Mkoa wa Dodoma Bw.Salum Shaban Salum amelitaka tawi jipya la umoja wa vijana wa CCM (UVCCM) la Chuo cha Uandishi wa Habari na Utangazaji Dodoma kuendeleza,kudumisha uzalendo pamoja na kuisemea Serikali kwa kazi zinazofanywa na Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dk.Samia Suluhu Hassan.

Salum aliyasema hayo Mei 31,23023 wakati wa uzinduzi wa tawi jipya la umoja wa vijana (UVCCM) ambapo alisema matarajio ya kufungua tawi hilo ni kuongeza nguvu ndani ya Chama cha hicho pamoja na kuwaandaa vijana kuwa wazalendo wa nchi ili kulinda amani,kuyasema yanayofanywa na serikali ya Jamuhuri ya Muungano.

Pia Salum aliyabainisha mafanikio yaliyofanywa na Serikali ya awamu ya sita hasa katika utekelezaji wa miundombinu mbalimbali hususani katika sekta ya Elimu,Barabara,Maji sanjali na hayo ameitaja miundombinu ya standard Gage,Uwanja wa Ndege wa kimataifa uliopo Jijini Dodoma na ukamilishaji wa majengo mbalimbali ya serikali.

“Niwazi kila mtu anayaona anayo yafanya Mama kazi yetu sisi kama vijana ni kuhakikisha tunamuunga mkono Mama katika shughuli za kimaendeleo amefungua mikutano ya siasa ndohivi vyama vipo katika siasa yote haya ni kwaajiri ya kuleta maendeleo ndani ya nchi yetu.

Nae Katibu wa Umoja wa Vijana Wilaya ya Dodoma Mjini Makao Makuu ya Serikali na Makao Makuu ya Chama cha Mapinduzi Bw.Issack Ngongi alisema kufuatia ufunguzi huo UVCCM watahakikisha wanaongeza wanachama ili kuwezasha kufanya shughuli za Chama na kuisaidia katika kuleta maendeleo.

Alisema wanachama hao wapya wanatakiwa kuja kujiunga na Chama hicho ni uzalendo huku akisema sera ya Chama cha Umoja wa Vijana wa CCM ni ujamaa na kujitegemea.

Kadharika Ngongi alisema Chama hicho kipya kinatakiwa kutambua majukumu yake hasa katika kuisemea Serikali mambo mbalimbali ikiwa ni pamoja na kumsaidia Rais Dk.Samia Suluhu Hassan majukumu,kuisapot Serikali ili kufikia adhima ya Iran ya Chama cha Mapinduzi CCM.

“Leo tumefungua tawi hili la Chuo cha Uandishi wa Habari na Utangazaji Dodoma kwahiyo tuhakikishe tunakuwa wamoja katika Wilayah ii ya Dodoma Mjini lakini kushirikiana na Seneti ya Mkoa kwa kushiriki katika shughuli za Chama na Serikali,”alisema

 


 

                            

 

Previous Post Next Post