WAJASILIAMALI KUANZISHA TUZO YA MAVUNDE DODOMA


Taasisi ya Chama cha wanawake Jijini Dodoma (WAUVI) inatarajia kuanzisha Tuzo ya Mavunde ya wajasiliamali itakayolenga kupata kikundi cha kuongeza thamani ya mazao na mifugo kitakacho pewa mitambo na mashine yenye thamani ya shilingi 20,000,000.

Hayo yalisemwa Mei 30,2023 na Naibu Waziri wa kilimo na Mbunge wa wa Jimbo la Dodoma mjini Mhe.Anthony Mavunde katika viunga vya Nyerere Squer Jijini Dodoma alipokuwa akifunga mafunzo ya wajasiliamali Mkoa wa Dodoma.

Mavunde alisema serikali inatambua jitihada zinazofanywa na wajasiliamali hususani katika utendaji wa shughuli za kimaendeleo ndani ya mkoa wetu huu wa Dodoma.

“Niwapongeze sana wanawake wa Dodoma na Chama kwa ujumla endeleeni kutoa elimu kuhusiana na ujasiliamali ili kuweza kutibu suala la umasikini katika jamii zetu tuwajibike kila mtu kwa nafasi yake bila kusahau malezi ya watoto wetu,”alisema  

Nae Mwenyekiti wa Chama cha Wanawake (WAUVI) Mkoa wa Dodoma Bi.Ester Said amesema lengo la Taasisi ya (WAUVI) ni kukuza Viwanda vidogovidogo,kupanua wigo wa kibiashara na masoko,kutoa mafunzo ya kielimu katika masuala ya kijamii,kitamaduni na kiafya,kuongeza kipato kwa mtu mmoja mmoja na maarifa kwa ujmla katika nyanja tofauti.

Alisema katika Taasisi ya (WAUVI) inatarajia kupunguza umaskini katika kaya maskini kwa wanawake,kupunguza wimbi la watoto wa mitaani huku ikiahidi kuwapa kipaumbele wanawake na watoto.

Pia aliwataka wanawake kuwasaidia waume zao shughuli mbalimbali ili kuondoa sintofahamu zinazojitokeza mara kwa mara ndani ya ndoa na badala yake kudumisha mahusiano ya kujenga jamii bora.

“Kwetu sisi fursa hii ujio wake umetupa faraja na matumaini makubwa pia tunatoa pongezi kwa wadu wote walioshiriki kwa wakati wote wa program hii ya Zunguka na Mama Samia.

“Ushirikii wao umekuwa chachu kwa ufanisi kwa program yote iliyotolewa kwa wajasiliamali wetu ni matumaini yetu kuwa wataendelea kuwa nasi ili kuendeleza miongozo muhimu kwa wajasiliamali wetu ili sote kwa pamoja tufikie ndoto ya kushiriki vyema uchumi wa Viwanda,”alisema

Hata hivyo Said alisema Taasisi hiyo imejipanga kusaidia serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt.Samia Suluhu Hassan katika kuende na kasi ya kupunguza ukosefu wa ajira nchini.

Alisema Taasisi hiyo imekuwa na idadi kubwa ya usindikaji wa bidhaa mbalimbali ndani ya Mkoa wa Dodoma na maeneo mengine huku akisema kuwa watu wameanza kupata mafunzo mbalimbali ya kuendesha shughuli zao za kibiashara nchini.

Aidha Said alisema Chama hicho hadi sasa kinawanachama takribani 3200 wanawake wakati idadi ya wanaume ikiwa ni 500 na kusema Taasisi hiyo halhijabagua jinsia kwa lengo la kuleta ushindani katika baadhi na kukuza soko la wajasilisiamali nchini.

Previous Post Next Post