SHIRIKA Umeme Tanzania (TANESCO) limeandika Historia ya kwanza kwa kusaini mkataba wa Mradi wa kuzalisha umeme kwa njia ya jua kwa kutumia Teknolojia ya Solar Photo Voltaic wenye uwezo wa kuzalisha megawati 150 za umeme.
Hayo yamesemwa leo Mei
29,mwaka huu katika Ukumbi wa Morena Jijini Dodoma na Waziri wa Nishati January
Makamba wakati wa hafla ya utiaji saini mkataba wa kwanza nchini wa kuzalisha
umeme wa jua megawati 50 utakao jengwa katika Wilaya ya Kishapu Mkoani
Shinyanga.
Pia ameseam hadi kukamilika
kwa mradi huo ikiwemo ulipaji wa fidia kwa watakaopisha eneo la mradi itaghalimu
jumla ya fedha kiasi cha shilling Bilioni 274.76.
Hali kadhalika awali
Mhe.Makamba ameeleza kuwa utekelezaji wa mradi huo unatarajiwa kuanza mwezi
juni mwaka huu ambapo utachukua takribani miezi 14 hadi kukamilika kwake.
Tags
HABARI