VITUKO VYA MASHABIKI YANGA HAISHIKIKI KESHO HATOKI MTU


 Yanga  watashuka  dimbani  leo  kumenyana  na   USM Alger  katika  mchezo  wa  kwanza  wa  Fainali  ya kombe  la shirikisho (CAF) dulu hilo litapigwa katika dimba la Benjamini Mkapa  Jijini Dar  es saalam.

Akizungumza na Mapinduzi Digital kwenye  uwanja  wa  shule  ya  Msingi  Nkuhungu  mmoja   wa shabiki wa  timu  hiyo  Efraim   Lumumba  amesema  timu  hio  imekuwa  na mwendelezo mzuri  tangu  msimu uanze  ivyo imekamilika   kila  idara.

  Amesema wachezaji wamepata  mda  wakutosha  kupumzika  baada   ya kucheza  mchezo  wao  wa nusu Fainali ya kombe la Azam Federation Cup Mkoani  Singida kwenye uwanja wa CCM Liti nakuibuka na ushindi wa bao 1-0  katika mchezo  wa nusu Fainali ya kwanza.

Amesema USM Alger wajiandae kuondoka wakilia nahuzuni nzito  watakapo ona wananchi wanapepelusha bendera ya kijani huku wakitetema kwenye uwanja wa Mkapa kwa sababu maandalizi ya timu hiyo yanalizisha lengo nikupata alama wakiwa katika Dimba la Mkapa.

"Katika mchezo huu tutahakikisha tunaonyesha uzalendo wetu wa kweli Usm Alger tutawafunga na tutaendelea kutunza historia ya kuchukua kombe la hili laundi hii tuna wapiga ndani nje kwetu tunabuluza natukienda kwao wembe ni uleule''alisema Lumumba.

Naye Carolina Masawe aliongeza kwa kusema kuwa maandalizi mazuri na uwajibikaji wa mchezaji mmojamoja unaweza ukatoa ushindi kwa pande zote mbili hivyo kama yanga wamejiandaa vizuri wataweza kupata matokeo.

Amesema yanga wasibweteke kwa sababu hawajui wapinzani wao wamejiandaa kwa nanmna gani kuelekea kwenye Fainali hiyo na watatumia mbinu gani kwa sababu hawajawahi kucheza nao mchezo wowote.

‘’USM Alger ninavyo wajua katika michezo yao mingi huwa wanatumia mbinu ya kujilinda sana ili wapinzani wao wasiweze kutikiswa nyavu zao kwahiyo wanajangwani kazi ipo na siyo kidogo''alisema masawe

 

 


Previous Post Next Post