ALIYEMPA KICHAPO NA KUMJERUHI MKE WAKE ARUSHA AKAMATWA


Jeshi la Polisi Mkoani Arusha limefanikiwa kumkamata mtuhumiwaa anaejulikana kwa jina la Isack Robertson mwenye umli wa miaka 45 na mkazi wa Sombatini Mkoani Arusha kwa tuhuma za kumpiga na kumjeruhi mke wake aitwae Jackline Mkonyi mwenye umli wa miaka 38 wa Sambotini Mkoani Arusha.

Hayo yamebainishwa leo 28 MEI,2023 na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha ACP Justine Masejo amesema Mtuhumiwa huyo ameendelea kuhojiwa na pindi upelelezi utakapo kamilika jarada litapelekwa Ofisi ya Taifa ya mashtaka kwa hatua zaidi za kisheria.

Jeshi la Polisi Mkoani humo limetoa onyo kwa baadhi ya watu wachache wanaofanya vitendo vya ukatili katika familia zao na sehemu nyingine kuacha mara moja huku likisema halitasita kuwakamata na kuchukuliwa sheria watakaobainika na vitendo hivyo.

“Niwaombe wananchi popote pale mlipo msifumbie macho vitendo viovu na pia musiache kutoa ushirikiano pindi mnapoon tukio lolote ambalo si jema ili jeshi la Polisi liweze kuwashughulikia waharifu na kukomesha vitendo hivi.

Previous Post Next Post