RAIS WA JAMUHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA AKIKATA UTEPE KUASHILIA UZINDUZI RASMI WA IKULU DODOMA KISHA KUTETA JAMBO NA VIONGOZI


 Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dk.Samia Suluhu Hassan amezindua rasmi Ikulu ya Chamwino iliyopo Jijini Dododma ambapo amesema kukamilika kwa jengo la Ikulu mpya ya ni matokeo ya kazi nzuri iliyofanywa kwa ushirikiano kati ya ofisi ya Ikulu,Wakala wa majengo Tanzania (TBA) na shirika la uzalishaji mali na Jeshi la kujenga Taifa (JKT).

Dk.Samia ameyasema hayo leo 20 Mei 2023 alipokuwa akizindua jengo mpya la Ikulu ya Chamwino iliyoko Jijini Dodooma akiambatana na viongozi wengine wa serikali akiwepo Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Zanzibar Dk.Hussein Ali Mwinyi,Makamu wa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dk.Philp Mpango,Waziri Mkuu Kassim Majaliwa Majaliwa,Marais wastaafu na Viongozi wengine.

Rais Samia amesema historia ya ujenzi wa Ikulu hiyo ni alama na uthibisho rasmi wa kukamilika kwa adhima ya serikali ya kuifanya Dodoma kuwa makao makuu ya serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania.

Pia amesema kufuatia ujenzi wa majengo ya serikali yaliyopo Msalato Jijini Dodoma katika ujenzi wa makao makuu watafika pia wageni wa mataifa mengine kisha kupokelewa kama ilivyo katika Ikulu ya Dar es salaam.


"Hatua kwa hatua Mji wa Dar tunauacha kuwa Mji wa biashara niwaombe sana viongozi wote tuwdumishe umoja na mshikamano pamoja na kufanya kazi kwa bidii ili Taifa letu liendelee kusonga mbele na uchumi ukuwe zaidi na kufikia uchumi wa kati na wa juu,nikupiti upendo wetu,umoja na mshikamano ndio maana matunda yameweza kuonekana.

Dk.Samia ametoa wito kwa Watanzania wote kuendana n
a mwenendo wa sasa upendo,maelewano na mshikamano ili kusaidia kuendeleza Taifa huku akisema waasisi wa taifa waliweka misingi imala ambayo itaendlea kudumishwa na kuimalishwa/

Rais.Samia amesema huduma zote zinazopatikana katika Ikulu ya Dar es salaam zitatolewa pia Dodoma yalipo makao makuu ya Tanzania.

Pamoja na hayo Dk.Samia amesema mchakato wa kuhamishia makao makuu ya serikali kutoka Dar es salaam kwenda Dodoma yalianza muda mrefu ambapo ulikuwa na mchakato wa kidemoklasia ambao mjadara mpaka kufikia uamzi umepitia ngazi mbalimbali za chama.




Akiwa katika hafla ya uzinduzi huo Rais Samia ameeleza kuwa mwaka 1966 Jeseph Nyerere ambaye ni mdogo wa Mwalimu Nyerere na aliyekuwa Mbunge wa Msoma aliwasilisha hoja binafsi Bungeni ya kutaka makao makuu ya serikali yahamishiwe Dodoma hata hivyo hoja hiyo ilipingwa na kuondolewa na badae mwaka 1972 April kamati tendaji ya TANU yMkoani Mwanza aliibua hija hiyo na kuliwasilisha pendekezo rasmi kwa kamati kuu ya chama hicho wakati kamati kuu ya chama cha TANU kilichoongozwa na Mwalimu Nyerere kisha kulidhia pendekezo hilo.

Amesema kamati kuu ya Chama cha TANU iliyoongozwa na Mwalimu Julius Nyerere iliadhimia kujadiliwa kwa pendekezo hilo katika matawi yote 1859 ya TANU yaliyokuwepo wakati huo ili kufanyiwa uwamzi huku matokeo yake yakielezwa kuwa matawi 1017 yaliunga mkono na matawi 842 yalipinga pendekezo hilo huku jitihada zikiendelea kutafutwa ili kukamilisha zoezi hilo.

Dk.Samia amesema kufuatia maagizo yaliyotolewa na Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere ambayo yemetekelezwa na viongozi marais wastaafu kila Rais kwa nafasi yake ingawa haikuwa ni rahisi kutokana na sababu mbalimbali hasa za kiuchumi jambo ambalo limefanya shughuli hiyo kuchukua muda murefu kukamilika kamailivyotarajiwa.


Nae Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi amepongeza juhudi zinazofanywa na serikali ya awamu ya sita hasa katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za kimaendeleo nchini.

Dk.Mwinyi amesema ameishukuru serikali kwa kuipatia serikali ya Zanzibar sehemu itakayotumika kujenga Ofisi za Serikali hiyo ili kuwawezesha watumishi kupata mazingira bora ya utendaji kazi.

Pia Dk.Mwinyi amesema katika Ikulu mpya imetengwa Ofisi ya Rais wa Zanzibar huku akiipongeza serikali kwa hatua hiyo pamoja na wote walioshiriki katika ujenzi wa Ikulu hiyo likiwemo Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) Mawakala wa majengo Tanzania na kuhakikisha ujenzi huo unakamilika kwa wakati.


Pamoja na hayo Makamu wa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dk.Philp Mpango amesema Ikulu hiyo imejengwa kwa nguvu zilizotokana na kodi za Watanzania huku akitoa maagizo kwa viongozi wa Ikulu kuliheshimu jengo hilo pamoja na kulitunza ili liweze kutoa maamzi sahihi na kumusaidia Mhe.Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dk.Samia Suluhu Hassan.

Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dk.Samia Suluhu Hassan katikati akiteta jambo na Rais wa Zanzibar na Mwenyeki wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussei Ali Mwinyi na Makamu wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dk.Philp Isidor Mpango mala baada ya kukamilisha zoezi la uzinduzi wa Ikulu ya Chamwino Jijini Dodoma.

           

Previous Post Next Post