MAAGIZO YA RAIS DK.SAMIA SULUHU HASSAN KWA MAWAZIRI NCHINI ATAKA NIDHAMU NA UBUNIFU



Rais wa Jamuhuri yanMuungano wa Tanzania Dk.Samia  amewataka Mawaziri kuendeleza nidhamu na ubunifu katika utekelezaji wa majukumu mbalimbali ili kuleta ufanisi katika maendeleo ya kitaaluma.

Rais Samia ameyasema hay oleo nchini Zanzibar aliposhiriki katika kuhitimisha mkutano wa kitaaluma wa chama cha makatibu mahususi na Menejimenti ya kutunza kumbu kumbu ya APRA na TAPSEA ambapo amewapongeza viongozi hao kwa kuendelea kusimamia sekta hiyo.

Dk.Samia pia amewasihii viongozi hao kuendelea kutatua changamoto zinapojitokeza huku akiwataka watumishi wa kada ya Elimu kuchangamkia fursa kwani inawajenga kitaaluma na kuwapa nafasi ya kupumzika.

Dk.Samia amewataka wafanyakazi kwenda sawa na viapo walivyo apa ili kuendelea kufanya kazi kwa ufanisi na kumtakaa Waziri wa utumishi na Waziri anaeshughulika na ajiri kuzungumza na waajiri kuyatekeleza vyema majukumu yao.

“Kama mwanadamu unataka kupumzika Mawaziri lishughulikieni hilo,nimesikiliza kiapo chenu hapa na mzlivyosema lakini hii ndio fursa pekee kwa kada hizi kutoka nje ya Ofisi zao wakitoka ni wakati wa likizo lakini likizo waenda Vijijini kwa wazazi kwa hiyo ile wapiti kupmzika wanapata matatizo tele yanawasubiri labda wananchopata ni kubadilisha mazingira tuu. 

Katika hatua nyingine Dk.Samia amewakumbusha na kuwataka kusimamia suala la kuongezwa kwa hadhi ya Chuo cha Utumishi Kampasi ya Tabora ambapo amesema awali yalitolewa maagizo ya kuongezwa hadhi ili kiweze kuandaa watendaji wenye uweledi na viwango vya juu.

Pia Rais Samia amempongeza Waziri kwa kukamilisha agizo hilo huku akimtaka kukamilisha suala la mitaala kwa wakati ili Chuo kianze kazi kama ilivyopangwa.

Amesema kuhusu Chuo cha Maarifa kilichopo Jijini Dodoma kitawekwa jina la Samia hadi pale ujenzi utakapo kamilika”Sisi waswahili hatutoi jina mpaka motto azaliwe si waswahili wa zamani,sasa subirini kituo hiki kikamilike tukione kilivyo tutaamua jina gani,”Dk.Samia

Aidha Dk.Samia amesema mfumo uliopo utaendelea kujenga taasisi imara.  

Previous Post Next Post