Rais Samia Suluhu Hassan ametangaza baraza jipya la mawaziri, likihusisha wizara 27, huku akitimiza ahadi yake ya kuunda wizara kamili ya vijana.
Kwa mujibu wa mkuu huyo wa nchi, wizara hiyo itakuwa chini ya ofisi yake na itaitwa Wizara ya Nchi, Ofisi ya Rais, Maendeleo ya Vijana na kwamba Joel Nanauka ameteuliwa kuiongoza.
Rais Samia ametangaza baraza hilo leo, Jumatatu Novemba 17, 2025 katika mkutano wake na waandishi wa habari, uliofanyika Ikulu ya Chamwino jijini Dodoma.
Sambamba na wizara hiyo, pia amefanya marekebisho madogo na kuunda Wizara ya Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira na Mahusiano.
“Atakayeshika nafasi hiyo atakuwa na kazi ya kufanya mazungumzo na makundi mbalimbali kuhakikisha mahusiano mazuri,” amesema.
Aidha, marekebisho mengine yameshuhudiwa katika Wizara ya Nchi Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) na sasa imehamishiwa Ofisi ya Waziri Mkuu.
Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
👔 Waziri - Mh. Ridhiwani Jakaya Kikwete
👩💼 Naibu - Regina Ndege Kwarai
Ofisi ya Rais Mipango na Uwekezaji
👔 Waziri - Prof. Kitila Mkumbo
👩💼 Naibu - Pius Steven Chaya
Ofisi ya Rais Maendeleo ya Vijana
👔 Waziri - Joel Nanauka
Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira
👔 Waziri - Mh. Mhandisi Hamadi Masauni
👩💼 Naibu - Dkt. Festo Dugange
Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu
👔 Waziri - Mh. William Lukuvu
👩💼 Naibu - Ummy Nderiananga
Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Ajira na Mahusiano
👔 Waziri - Mh. Deus Sangu
👩💼 Naibu - Mh. Rahma Riadh Kisuo
Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
👔 Waziri - Mh. Prof. Riziki Sailas Shemdoe
👩💼 Naibu - Mh. Reuben Nhamanilo (Elimu)
👩💼 Naibu - Mh. Dr. Jaffar Rajab Seif (Afya)
Wizara ya Fedha
👔 Waziri - Mh. Balozi Khamis Musa Omar
👩💼 Naibu - Mh. Laurent Deogratius Luswetula
👩💼 Naibu - Mh. Mshamu Ally Munde
Wizara ya Mambo ya Nje
👔 Waziri - Mahmood Thabit Kombo
👩💼 Naibu - Dkt. Ngwaru Jumanne Magembe
👩💼 Naibu - Mh. James Kinyasi Millya
Wizara ya Mambo ya Ndani
👔 Waziri - Boniface Simbachawene
👩💼 Naibu - Denis Lazaro Londo
Wizara ya Kilimo
👔 Waziri - Daniel Chongolo
👩💼 Naibu Waziri - Mh. David Silinde
Wizara ya Maji
👔 Waziri - Mh Juma Aweso
👩💼 Naibu Waziri - Mh. Kundo Andrew Mathew
Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa
👔 Waziri - Mh. Raymond Simon Nyansao
Wizara ya Ujenzi
👔 Waziri - Abdallah Ulega
👩💼 Naibu - Mh. Godfrey Msonge
Wizara ya Uchukuzi
👔 Waziri - Prof Makame Mbarawa
👩💼 Naibu - Mh. David Mwakiposa
Wizara ya Viwanda na Biashara
👔 Waziri - Mh. Judith Salvio Kapinga
👩💼 Naibu - Mh. Patrobas Katambi
Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari
👔 Waziri - Mh. Angela Kairuki
👩💼 Naibu - Mh. Sweetbert Zakaria Mkama
Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum
👔 Waziri - Dorothy Gwajima
👩💼 Naibu - Mh. Marry Mahundi
Wizara ya Afya
👔 Waziri - Mohammed Mchengerwa
👩💼 Naibu - Dkt. Florance George Samizi
Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia
👔 Waziri - Prof. Adolf Mkenda
👩💼 Naibu - Wanu Hafidh Ameir
Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi
👔 Waziri - Dkt. Leonard Akwilapo
👩💼 Naibu - Kasper Kasper Muya
Wizara ya Mali Asili na Utalii
👔 Waziri - Mh. Asha Kijaji
👩💼 Naibu - Hamad Hassan Chade
Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo
👔 Waziri - Prof. Palamagamba Kabudi
👩💼 Naibu - Hamisi Mwinjuma
👩💼 Naibu - Paul Makonda
Wizara ya Mifugo na Uvuvi
👔 Waziri - Dkt. Bashiru Ally Kakurwa
👩💼 Naibu - Mh. Ngwasi Damas Kamani
Wizara ya Madini
👔 Waziri - Anthony Peter Mavunde
👩💼 Naibu - Mh. Dkt. Steven Lemomo Kiruswa
Wizara ya Nishati
👔 Waziri - Mh. Deogratius Ndejembi
👩💼 Naibu - Salome Makamba
Wizara ya Katiba na Sheria
👔 Waziri - Mh. Juma Homera
👩💼 Naibu - Zainab Athuman Katimba
