Marekani ipo kwenye majadiliano ya kuwekeza mabilioni ya dola katika sekta kubwa ya madini ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, wakati huo huo ikitaka kuunga mkono juhudi za amani mashariki mwa nchi hiyo yenye migogoro Kulingana na shirika la habari la Reuters, mpango huo ambao bado unaandaliwa, ulifichuliwa wakati wa ziara ya ngazi ya juu ya Massad Boulos, mshauri mkuu wa Afrika kwa Rais wa Marekani Donald Trump.
Akizungumza baada ya mkutano na Rais wa Kongo Felix Tshisekedi mjini Kinshasa, Boulos alisema Washington imechunguza pendekezo la madini ya DRC kwa ajili ya usalama na kukubaliana juu ya njia ya kusonga mbele.
Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) ni mojawapo ya mataifa yenye utajiri mkubwa wa madini duniani, ikiwa na akiba ya cobalt, lithiamu, uranium, na madini mengine muhimu muhimu kwa magari ya umeme na teknolojia ya simu.
Sehemu kubwa ya pato la sasa la chimbaji madini chini Congo linatawaliwa na makampuni ya China lakini hivi karibuni Marekani imeonyesha nia ya dhati ya kimarisha hamu yake kutafuta madini ya kimkakati.
'Umesikia kuhusu mkataba wa madini. Tumepitia pendekezo la Congo, na rais na mimi tumekubaliana juu ya hatua zitakazochukuliwa, Boulos aliwaambia waandishi wa habari, kama livyotajwa na Reuters.
Ingawa maelezo mahususi ya mango huo bado hayajafichuliwa, Boulos alionyesha kuwa makampuni ya sekta binafsi ya Marekani yatakuwa muhimu kwa ushirikiano wowote.