BUNGE LA TANZANIA LASHIRIKI KIKAMILIFU KUKUZA UHURU WA HABARI HAPA NCHINI

 


Na Stella  Ngenje,Songea.


Mbunge wa Jimbo la Madaba Wilayani Songea Mkoani Ruvuma Mhe Dkt. Joseph Kizito Mhagama, amesema Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania limeshiriki Kukuza Uhuru wa Habari hapa Nchini kwa Kutunga Sheria ya Huduma za Habari Sura ya 229 Pamoja na Marekebisho ya Sheria hiyo ya Mwaka  2023.


Mhe. Mhagama ameyasema hayo Jijini Arusha  akishiriki Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Habari yanayofanyika Wiki hii katika Jiji hilo la Kaskazini mwa Tanzania. 


Mbunge wa Madaba akipigilia  Msumari kuhusu Ushiriki wa Bunge, ameeleza kwamba Maboresho ya Sheria hiyo ya Mwaka 2023, yanawataka Waandishi wote wa Habari kuwa na Kiwango Cha Elimu  Kinachoanza na Taaluma ya Diploma Kwa Kipindi Cha Miaka 5 tangu Marekebisho hayo Kufanyika Mwaka 2023,hatua hiyo itawezesha kuongeza Hadhi ya Tasnia ya Habari hapa Nchini, nakuondoa Ukanjanja Kwenye Tasnia hii Muhimu. 


Ikumbukwe kuwa Mhe. Dkt. Joseph Kizito Mhagama Licha yakuwa ni Mbunge wa Jimbo la Madaba, lakini pia ni Mwenyekiti wa Bunge la Tanzania, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge  Utawala Katiba na Sheria, ni Miongoni mwa Wabunge Wachache  wanaoliwakilisha Bunge la Tanzania Kwenye Bunge la Dunia, linaloongozwa na Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani ambaye pia ni Spika wa Bunge la Tanzania   Mhe. Dkt. Tulia Ackson.


🚨Subscribe YouTUBE Channel yetu ya WASHINDI MEDIA.

Previous Post Next Post