NG'OMBE WA KILO 1000 AWA MVUTO WA PEKEE MAONESHO YA NANENANE


 Wellu Mtaki, Dodoma .

Nyasi asili inayokua kwenye maeneo ya jangwa au nusu jangwa na  kupandwa kwenye maeneo yenye ukame Ant grass  inasaidia kukuza Mifugo aina ya Ng'ombe.


Hayo yamebainishwa na  Afisa Uvuvi wa halmashauri ya Wilaya ya Itigi mkoani Singida Pascal  Maiko Peter wakati akizungumza na vyombo vya habari Jijini Dodoma Katika maonesho ya nanenane huku akiwataka wananchi kutembelea Banda la halmashauri hiyo kujionea Ng'ombe mwenye kilo zaidi ya 1000 anayeleta maajabu Katika maonesho hayo.


Amesema licha ya Mifugo ya Ng'ombe pia wapo Mifugo mingine ikiwemo Ufugaji wa samaki, kuku, Bata pamoja na Sungura.



"Ant grass" kwa malisho ya Ng'ombe kwa kawaida humaanisha nyasi aina ya Anthephora pubescens - nyasi ya asili inayokua sana kwenye maeneo ya jangwa au nusu jangwa, hasa kusini mwa Afrika, lakini pia hupandwa kwenye maeneo yenye ukame kama malisho" amesema.


Aidha ameeleza kuwa mkoa wa Singida hakuna ziwa Wala mito ila wanatumia mabwawa kwa ajili ya Ufugaji wa samaki  na kusaidia kupata  maendeleo endelevu kwa kujiongezea kipato kwa mtu mmoja mmoja na kuondoka umasikini .


Mbali na hayo amesema kuwa huduma ya chanjo inapatikana bure kwa mteja ambaye atachukua Mfugo aina ya kuku hivyo amewaasa wafugaji kutembela Banda hilo Ili kupata Elimu zaidi.





🚨Subscribe YOUTUBE Channel Yetu ya WASHINDI MEDIA.

Previous Post Next Post