Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe. Jumanne Sagini (Mb) amefungua semina ya Siku Tano yenye lengo ya kubadilishana uzoefu wa namna ya kudhibiti ajali na kuwa na usalama barabarani ili kuondokana na madhira yanayoikumba jamii ikiwemo vifo na ulemavu.
Akizungumza wakati akifungua semina ya siku tano Novemba 27 hadi Disemba 2, mwaka huu ya Kanda ya Afrika kuhusu mpango wa usalama barabarani iliokutanisha nchi mbalimbali ikiwemo Tanzania, Afrika Kusini, Burundi, Rwanda na Botswana iliondaliwa na Shirika lisilo la kiserikali linalohusika na utoaji wa elimu ya usalama barabarani la Tanzania Safety Roads Initiatives (TARSI) ameeleza kuwa ajali nchini zimepungua.
"Ajali za barabarani zimepungua ila sio kama awali na tunaendelea kudhibiti kwani mara nyingi zinatokana na sababu za kibinadamu kama dereva mwenyewe pia kuna matatizo ya vyombo vya moto vyenyewe, uchakavu na ubovu pamoja na miundombinu kuwa mibovu," amesema.